Sunday, December 1, 2013

MIRATHI YA KAKA sehemu ya 50

KWA WASOMAJI WAPYA......
Brighton anaota ndoto ya ajabu akiwaona watu waliokufa siku nyingi kwa kujiua wakiwemo mzee Mboma, Patrick, James na Anna. Baada ya ndoto hiyo anazongwa na mwanadada Sharifa anayemsababishia kesi ya mauaji ya mpangaji wake, yaani Kishoka. Kesi inaunguruma mahakamani kisha anajikuta akihukumiwa adhabu ya kunyongwa mpaka afe kwa kosa la mauaji ya Kishoka, kosa ambalo alikuwa hajalitenda. Akiwa gerezani akisubiri tarehe za kunyongwa anakutana na Mack, jamaa aliyekuwa amenunua nyumba iliyokuwa ya marehemu James, naye Mack anaanza kumhadithia kisa kilichompelekea afungwe jela.
Kwa kusimuliwa na Mack, Brighton anayasikia mengi kuhusu mali alizokuwa amerithi kutoka kwa marehemu kaka yake kwa kila aliyekuwa amemuuzia aliishia kupatwa na matatizo akiwemo Mack mwenyewe. Hatimaye siku ya kunyongwa inafika kweli, hata hivyo anajikuta anakolewa kimiujiza na msichana aliyemsingizia kuua, yaani Sharifa, anatolewa gerezani na kuwa huru kabisa.
Anaporudi kwake anakuta nyumba yake ishauzwa na mtu aliyekuwa amemwachia.  Anaamua kwenda kwa jamaa yake na huyo mtu kumuulizia naye anaambiwa jamaa huyo katimkia Afrika ya kusini.

ILIPOISHIA TOLEO LILLOPITA...
Nilipomaliza kula mazungumzo yalianza. Shauku yangu kubwa ilikuwa ni kusikia habari za Mapara. Hata hivyo kwa wakati huo nilikuwa na uhakika wa kusikia habari zote za Mapara kutoka kwa Benja kwani ukaribu wao ulikuwa ni kama pete na chanda.
SASA ENDELEA..........
           
Alianza kwa kunipa pole kwa matatizo yote yaliyokuwa yamenisibu. Baada ya hapo alianza kunieleza habari niliyokuwa naingijea kwa hamu kubwa.
            “Tangu upatwe na matatizo Mapara alikuwa akijitahidi sana kuisimamia miradi yako. Tena ilikuwa ikiendelea vizuri kila kukicha.” Alinieleza Benja.
            Wakati huo nilikuwa makini kusikiliza; hatua kwa hatua, neno kwa neno huku nikiwa na maswali tele kichwani juu ya hatima ya mali zangu baada ya kudokezwa kuwa niliyekuwa nimemwachia dhamana ya kuziangalia na kuzitunza alikuwa katimkia ughaibuni.
            Benja aliendelea kunieleza kuwa baada ya hukumu yangu Mapara alianza kujitapa kuwa mali zote hizo nilikuwa nimemkabidhi. Akawa na jeuri ya pesa kupindukia, si unajua tena baadhi ya watu wanapopata pesa kirahisi rahisi huwa hawana machungu nazo!
            Akawa ni mtu wa ahasa. Wanawake na yeye, tena akawa anawabadilisha kama nguo. Mchana yupo na huyu, asubuhi alikuwa na yule na usiku utamuona na mwingine. Pombe na yeye kila wakati.
            Baada ya kutapanya mali kwa miezi kadhaa uchumi wa miradi yangu ulianza kushuka. Ndipo alipoanza kuuza kila kitu ili atimkie Bondeni kwa mzee Madiba, yaani Afrika ya kusini.
            Alimalizia kwa kuuza nyumba yangu akamuuzia kigogo mmoja ambaye alikuwa ni mbunge. Baada ya kukamilisha uuzaji wa nyumba yangu Mapara alikwea ‘pipa’ na kuishia ‘Sauzi’. Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa habari ya Mapara kwa mujibu wa maelezo ya Benja.
            Kichwa changu kilizidi kuwa kizito utadhani kilikuwa kimeng’atwa na manyigu. Sikutegemea kabisa kama Mapara angefanya utumbo kama ule.
            Mpaka hapo mipango yangu yote ilikuwa imechemka, kwa msemo wa vijana wa kileo ilikuwa ‘imebuma’. Niliendelea kupiga miayo mfululizo utadhani sijala siku tatu wakati ndiyo nilikuwa nimemaliza kushindilia sahani ya ubwabwa..
            “Sasa utanisaidiaje rafiki yangu, maana sitaki kabisa kuendelea kuishi kwenye mji huu kwani watu wanaweza wakasanua ishu kuwa nimetoroka jela.” Nilimuuliza Benja kwa sauti ya huruma.
“Kwa hiyo unataka ukaishi mji upi?”
“Mji wowote ule ilmradi uwe upo mbali na huu, nchi yetu ina miji mingi tu ambayo shughuli za kiuchumi zinapatikana. Nina imani nikifika sehemu na kutulia baada ya muda fulani mambo yangu yatakaa sawa.” Nilizidi kumweleza Benja.
            Pamoja na kuwa nilikuwa nipo mikononi mwake nikiamini kabisa kuwa shida yangu itafanikiwa, mambo yalizidi kuwa si mambo. Msaada wake ulikuwa si zaidi ya kunihifadhi kwa siku kadhaa ambazo ningekaa kwake. Kuhusu suala la pesa alikuwa ni mtupu.
            Sikushangaa kusikia hivyo kwa kijana huyo kwani tangu sijaenda jela maisha yake yalikuwa yapo vilevile. Pamoja na kukaa miaka lukuki jela bado nilimkuta hajaongeza hata stuli kwenye chumba chake hicho zaidi ya godoro la kulalia na redio kaseti aliyokuwa nayo.
            Hii yote ilitokana na kutojishughulisha katika maisha yake. Si yeye peke yake bali kulikuwa na vijana wengi tu katika mji huo waliokuwa na kasumba ya kukusanyikana kwenye masikani zao tu na kuanza kucheza kamali kutwa nzima.
            Baada ya kukosa msaada kwa mwenyeji wangu huyo nilikaa kimya kama dakika kumi hivi nikitafakari la kufanya ili kukimbilia kujificha kwenye mji mwingine tofauti na huo. Mapara alikuwa kashaniponza kwa kuyapeleka kombo mambo yangu yote.
            Kabla hatujafikia muafaka juu ya sakata langu, mlango wa chumba cha Benja uligongwa. Moyo wangu ulilipuka ‘lipu’ huku hofu ya kukamatwa ikitanda katika mawazo yangu.
Naye Benja aliinuka taratibu na kwenda kufungua mlango kidogo kidogo kisha akatoka kumsikiliza aliyekuwa anagonga.
Sauti ya msichana niliisikia ikimsalimia Benja kisha kumhoji ikimuuliza kama nilikuwemo ndani. Mapigo ya moyo yalizidi kwenda kasi baada ya kusikia jina la Brighton likitajwa, yaani jina langu.
Ilikuwa hainipi kabisa akilini kwa mtu mwingine yeyote katika mtaa huo au mji kwa ujumla kujua kuwa nilikuwa nimetoka jela. Sasa kitendo cha mtu kuja moja kwa moja na kugonga nilipokuwa nimefikia kisha kuniuliza kilikuwa kimenikosesha kabisa amani moyoni.
Nilibaki nikiomba kimungu mungu wasije wakawa askari polisi ama wana usalama. Nilijikuta nikiogopa hata kupumua kwa kuhofia mihemo yangu kusikika huko nje ya chumba.
Mara nilimsikia Benja akimhoji mtu aliyekuwa akiniulizia kuwa ni nani na alikuwa akinitafutia nini. Hata hivyo majibu ya msichana huyo sikuyasikia kwani alikuwa akiongea polepole sana.
“Huyo Brighton unayemuulizia haishi hapa wala mimi simjui. Kwanza hilo jina ni geni kabisa katika mtaa wetu, kama vipi endelea kuulizia kwa wengine.” Nilimsikia Benja akijibu hivyo.
Moyo wangu ulifurahi sana kusikia Benja akijaribu kupapatua ili kuokoa maisha ya uhai wangu uliokuwa umebaki. Hata hivyo mabishano makali yaliibuka baina ya mwanadada huyo na Benja.
Mwanadada huyo alikuwa akidai kuwa ana uhakika wa asilimia mia moja kuwa nilikuwemo chumbani humo huku Benja yeye akikanusha vikali.
Alirudi ndani haraka huku akiwa na hasira kisha akaufunga mlango kwa kuukomea ili kumkomoa mtu aliyekuwa akileta ubishi pale mlangoni. Sikutaka kumuuliza chochote kwani kama ningeongea basi sauti yangu ingesikika na kisha mpango wetu kubumbuluka.

HUYU MWANAMKE NAYE SASA ANATAKA KULETA BALAA KWA BRIGHTON! JE, NI NANI HUYO NA ANASHIDA GANI NA BRIGHTON? 

1 comment:

  1. UTAJIRI AU MALI ZA NDAGU NA MAJINI NDANI YA MASAA 48 MPAKA 72. KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA MAFANIKIO.
    Everyone
    Leo Natoa somo bure kuhusu Mali za ndagu,
    Unaweza kujiuliza mali za NDAGU ni nini?

    Dokta Mdiro call/whatsup +255 742162843.

    Ndagu ni dawa ambazo hutengenezwa kwa mkusanyiko wa taratibu fulani ambazo hufanyika kwa pamoja ikilenga jambo fulani.

    Hasa malengo makuu ya ndagu ni
    1.kutengeneza mali
    2.kulinda Mali.

    Ndagu hizi hutumia nguvu ya wazee(Mizimu)
    Sasa yapo nikupe maana ya mizimu ni nini?

    MIZIMU NI NINI?

    Mizimu ni roho za wazee wetu (wa ukoo) toka katika pande zote mbili Baba na Mama ambao ni babu na bibi toka kwa baba na babu na bibi toka kwa Mama,roho hizi huja na kuwa na sisi pale tunapozihitaji au zinapotuhitaji....!
    kwanini Mizimu huja kwetu au kwaini tunaiita?
    -UDUGU, kumbuka roho hizi ni zile za waze wetu (ancestors) ambao walizaa baba na mama zetu hivyoo kuja au kuwaita hutokana na Udugu

    ULINZI, roho zote zisizo na mwili huona yasiyoonekana kama Uchawi na magonjwa hivyoo Wazee wetu huja na tunawaita watuambie haya tusiyoyaona.

    MILA, utamaduni na desturi zetu hututaka tufanye mambo yaliyo katika mpangilio ulio sahihi kama kuwapa wazee heshima na kusikiliza yale wanayotuambia.

    Wazee hawa hutupatia mali kama zawadi lakini kwa masharti fulani maalumu hii ni tofauti na majini.

    Aina za ndagu zipo sita kunazile ambazo unaweza kufanya sehemu ulipo na zile ambazo unaweza kufanya kwa kunifuata yaani tukiwa pamoja hii ni kutokana na sababu mbalimbali kama wengine kutokuwa na ghalama za safari hivyo unaweza kufanya sehemu ulipo na jambo lako kukamilika.

    Ndagu ambazo ni lazima tuwe pamoja ni 4.
    1.Kutoa kitu.
    2.Mimba.
    3.Utasa.
    4.Ndugu 3.

    Ndagu ambazo unaweza kufanya sehemu ulipo ni 2.
    1. Ulemavu.
    2.Wanyama.

    Angalizo!!! Kwa msaada piga simu husijaribu jambo bila maelekezo ya dhati.

    Karibu sana na uwe na nia ya dhati.

    DOKTA MDIRO Namba call/whatsup +255 742162843

    ReplyDelete