Monday, November 25, 2013

MIRATHI YA KAKA sehemu ya 47

Brighton anaota ndoto ya ajabu akiwaona watu waliokufa siku nyingi kwa kujiua wakiwemo mzee Mboma, Patrick, James na Anna. Baada ya ndoto hiyo anazongwa na mwanadada Sharifa anayemsababishia kesi ya mauaji ya mpangaji wake, yaani Kishoka. Kesi inaunguruma mahakamani kisha anajikuta akihukumiwa adhabu ya kunyongwa mpaka afe kwa kosa la mauaji ya Kishoka, kosa ambalo alikuwa hajalitenda. Akiwa gerezani akisubiri tarehe za kunyongwa anakutana na Mack, jamaa aliyekuwa amenunua nyumba iliyokuwa ya marehemu James, naye Mack anaanza kumhadithia kisa kilichompelekea afungwe jela.
Kwa kusimuliwa na Mack, Brighton anayasikia mengi kuhusu mali alizokuwa amerithi kutoka kwa marehemu kaka yake kwa kila aliyekuwa amemuuzia aliishia kupatwa na matatizo akiwemo Mack mwenyewe. Hatimaye siku ya kunyongwa inafika kweli, hata hivyo anajikuta anakolewa kimiujiza na msichana aliyemsingizia kuua, yaani Sharifa, anatolewa gerezani na kuwa huru kabisa.  Sasa endelea...................

            ‘Ina maana Mapara keshakuwa mbunge siku hizi, au ndiyo ile tabia ya kujiweka ‘matawi ya juu’ na kulazimisha uheshimiwa pale mtu anapozinyaka.’ Nilizidi kuwaza huku nikitafuta majibu ya kumpatia jamaa huyo aliyekuwa kavimbisha tumbo lake kwenye kimlango kidogo cha geti langu.
            Kwa kweli ilikuwa ikiniwia ugumu jinsi ya kuanza kuuliza kuhusu huyo mhesimiwa aliyekuwa anasemwa yuko nje ya nchi. Wazo la kwamba Mapara keshakuwa mtu mkubwa kiasi kwamba mpaka akafikia hatua ya kuitwa mheshimiwa; lilikuwa haliniijii kabisa akilini.
            Mapara alikuwa hajasoma sana kiasi cha kuweza kugombea hata udiwani. Alikuwa kaishia darasa la saba tu, tena la saba lenyewe alikuwa ni ‘bongo lala’ kitu ambacho asingeweza kugombea kutokana na mabadiliko ya utandawazi tuliyonayo siku hizi.
            Siku hizi udiwani ni kuanzia ‘form four’, tofauti na siku za nyuma ambapo utamkuta diwani darasa la saba. Mambo yamebadilika, watu wameshaupumuzisha uongozi wa kianalogia na sasa hivi ni mwendo digitali mpaka kwenye umwenyekiti wa kitongoji ama umwenyekiti w serikali za mtaa.
            Sababu hiyo ndiyo ilizidi kuweta fukuto ndani ya kichwa changu. Nikawa nashindwa nianze vipi kuuliza habari za huyo Mapara niliyekuwa nimemuachia nyumba yangu pamoja na miradi yangu yote.
            “Kwani hapa ni kwa nani?” Nilijikuta naropoka kuuliza.
Jamaa aliguna kwanza kisha akasema,
“Watu wengine sijui mkoje, kwa hiyo wewe wakati unatoka huko ulikuwa unajua hapa ni kwa nani?” Swali hilo lilielekezwa kangu.
            Akili yangu ilizidi kukorogeka na kuvurugika. Nikajikuta nimeropoka tena,
“Kwani Mapara ndiyo mwenye nyumba hii?”
“Siyo bure wewe ni zuzu, maana tangu umefika sijaelewa hata kimoja unachoniambia. Hebu nenda moja kwa moja kwenye pointi yako ya msingi iliyokuleta hapa.” Alimaka jamaa huyo.
            Nikaona alichokuwa amekiongea ni kitu cha msingi, nikaona niende moja kwa moja kwenye pointi. Hata hivyo nilikuwa naogopa kumwambia kuwa nimeponea chupuchupu kunyongwa nikihofia siri itafichuka.
            “Sikiliza kaka, mimi ni mwenyeji kabisa wa mji huu ila nilitoka miaka kadhaa iliyopita. Sasa wakati natoka aliyekuwa akiishi hapa ni jamaa mmoja Mapara, la sijui mpaka sasa anakaa hapa?”
“Alaaha! Sasa nimekusoma. Hapa haishi huyo Mapara unayemsema, hapa ni kwa mheshimiwa mbunge na ni mwaka wa tatu sasa anaishi hapa, huyo uliyemtaja mimi hata simjui.”
             Kauli hiyo ilinifanya niishiwe nguvu. Nilizidi kuchoka. Mtu pekee ambaye nilikuwa nikitegemea aje awe msaada mkubwa kangu alikuwa ni Mapara, naye nilikuwa nimemkosa. Mtihani uliofuata ni wa kujiuliza pa kumpata.
            Wakati wa sakata la kifo cha Kishoka, Mapara alikuwa ndiyo mtu pekee aliyekuwa anakuja kunisalimia kituo cha polisi pamoja na kuniletea chakula. Hata nilipohamishwa na kupelekwa mahabusu ya magereza aliendelea kuwa anakuja kuniona.
Ndipo nilipomkabidhi funguo za nyumba yangu pamoja na majukumu mengine ya kusimamia miradi yangu.
            Hakuwa rafiki yangu ki vile japokuwa tulikuwa tunafahamiana sana kwa vile yeye ndiye alikuwa mmoja wa watu walionipokea kwenye mtaa huo wakati nahamia.
            Baada ya kuambiwa hivyo nikawa njia panda. Nikaanza kujiuliza sijui niende alipokuwa akiishi kwa kipindi kile ambapo alikuwa amepanga chumba kwenye nyumba moja iliyokuwa na wapangaji lukuki!

JE, NINI KITAFATIA? USIKOSE....

1 comment:

  1. UTAJIRI AU MALI ZA NDAGU NA MAJINI NDANI YA MASAA 48 MPAKA 72. KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA MAFANIKIO.
    Everyone
    Leo Natoa somo bure kuhusu Mali za ndagu,
    Unaweza kujiuliza mali za NDAGU ni nini?

    Dokta Mdiro call/whatsup +255 742162843.

    Ndagu ni dawa ambazo hutengenezwa kwa mkusanyiko wa taratibu fulani ambazo hufanyika kwa pamoja ikilenga jambo fulani.

    Hasa malengo makuu ya ndagu ni
    1.kutengeneza mali
    2.kulinda Mali.

    Ndagu hizi hutumia nguvu ya wazee(Mizimu)
    Sasa yapo nikupe maana ya mizimu ni nini?

    MIZIMU NI NINI?

    Mizimu ni roho za wazee wetu (wa ukoo) toka katika pande zote mbili Baba na Mama ambao ni babu na bibi toka kwa baba na babu na bibi toka kwa Mama,roho hizi huja na kuwa na sisi pale tunapozihitaji au zinapotuhitaji....!
    kwanini Mizimu huja kwetu au kwaini tunaiita?
    -UDUGU, kumbuka roho hizi ni zile za waze wetu (ancestors) ambao walizaa baba na mama zetu hivyoo kuja au kuwaita hutokana na Udugu

    ULINZI, roho zote zisizo na mwili huona yasiyoonekana kama Uchawi na magonjwa hivyoo Wazee wetu huja na tunawaita watuambie haya tusiyoyaona.

    MILA, utamaduni na desturi zetu hututaka tufanye mambo yaliyo katika mpangilio ulio sahihi kama kuwapa wazee heshima na kusikiliza yale wanayotuambia.

    Wazee hawa hutupatia mali kama zawadi lakini kwa masharti fulani maalumu hii ni tofauti na majini.

    Aina za ndagu zipo sita kunazile ambazo unaweza kufanya sehemu ulipo na zile ambazo unaweza kufanya kwa kunifuata yaani tukiwa pamoja hii ni kutokana na sababu mbalimbali kama wengine kutokuwa na ghalama za safari hivyo unaweza kufanya sehemu ulipo na jambo lako kukamilika.

    Ndagu ambazo ni lazima tuwe pamoja ni 4.
    1.Kutoa kitu.
    2.Mimba.
    3.Utasa.
    4.Ndugu 3.

    Ndagu ambazo unaweza kufanya sehemu ulipo ni 2.
    1. Ulemavu.
    2.Wanyama.

    Angalizo!!! Kwa msaada piga simu husijaribu jambo bila maelekezo ya dhati.

    Karibu sana na uwe na nia ya dhati.

    DOKTA MDIRO Namba call/whatsup +255 742162843

    ReplyDelete