ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA...
Kumbe
kulikuwa na mipango kabambe ya kumwingiza kipenzi changu kwenye jaribu zito
lililokuja kupelekea kifo chake.
SASA ENDELEA.......
Kuna kijana mmoja
ambaye alikuwa akimtaka Anna kimapenzi siku nyingi lakini ikashindikana. Kwenye
hicho kisherehe naye alikuwepo.
Baada ya kumuona Anna
kijana kijana huyo akasema kuwa lazima lengo lake litimie, ndipo
alipomchanganyia dawa za kulewesha kwenye soda na hatimaye akalewa na akawa
hajielewi.
Baada ya kufanya
hivyo kijana huyo alijichukulia mzigo kiulaini na kwenda kuutumia jinsi
alivyotaka. Lengo lake lilikuwa ni kufanya mapenzi na Anna, kweli alifanikiwa
japokuwa Anna alikuwa hajitambui.
Tukio hilo
lilimuumiza sana kipenzi changu. Hata hivyo wakati huo mimi nilikuwa masomoni
hivyo hakuweza hata kupata faraja kutoka kwangu. Miezi miwili baadaye tulifunga
shule. Ndipo niliporudi nyumbani na kukuta habari za kubakwa kwa Anna ambazo
ziliurarua moyo wangu.
Tunu ya usichana wa
Anna ambayo alikuwa ameitunza kwa ajali yangu ilikuwa tayari imeshahujumiwa.
Hakuwa bikira tena. Iliniuma sana kusikia hivyo. Hata hivyo sikutaka kuukatisha
uhusiano wetu kwa sababu ya hilo, nilimwambia kuwa tutakuwa pamoja licha ya
kwamba tunu yangu ilikuwa imeshahujumiwa.
Ndipo nilipomshauri
aende kuangalia afya yake huenda siku hiyo alipata maambukizi ya virusi vya
UKIMWI. Naye bila ubishi alienda, hata hivyo majibu yalikuwa safi.
Siku kadhaa zilipita.
Nikiwa sijui hili wala lile nilipokea taarifa za kifo cha Anna, taarifa ambazo zilizidi
kuuchoma moyo wangu.
Taarifa hizo zilisema
kwamba Anna alikuwa amekufa baada ya kufanya jaribio la kutoa mimba.
Niliposikia hivyo nilijua moja kwa moja mimba hiyo iliingia siku ile alipobakwa
na yule kijana.
Ndipo nilipozidi
kuumia na kujihisi mpweke zaidi ya kinda lililoachwa na mama likabaki peke yake
kwenye kiota. Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha ya Anna kwa hapa duniani
ingawa mpaka leo moyoni mwangu yu hai.
Tukio hilo liliniacha
na kidonda kikubwa sana ndani ya moyo wangu. Mpaka nakuja kuondokewa na kaka
yangu kidonda hicho kilikuwa hakijapata hata dalili za kupona, kikawa
kimegongomewa msumari mwingine tena mkubwa zaidi.
Aliyekuwa mstari wa
mbele kunifariji juu ya machungu ya kuondokewa na Anna naye alinitoka, tena kwa
kifo cha ghafla ghafla huku nikimshuhudia wakati roho inaachana na mwili wake.
Hakika lilikuwa ni pigo mjaarabu.
Huku nikiwa na
majonzi yangu tele moyoni niliendelea kulisongesha huku nikipata faraja kutoka
kwa majirani na rafiki zangu wa karibu, faraja ambayo hata haikukidhi mahitaji
ya upweke uliokuwepo ndani ya moyo wangu.
Kitu kingine ambacho
kilianza kuniacha hoi ni hizo mali zilizokuwa zimeachwa na kaka James. Nilizidi
kuchanganyikiwa kwa jinsi zilivyokuwa zikipukutika na kuisha bila kuelewa
zinaishaje.
Biashara zote zikawa
haziendi. Nikienda kwenye maduka mauzo yalikuwa mabovu, kampuni ya usafirishaji
nayo ikazidi kufilisika siku hadi siku. Ajali za mara kwa mara zikawa zinatokea
kwenye malori ya kusafirisha mizigo kwanye kampuni hiyo. Nilizidi kuchoka.
Baada ya kuona mambo
yanazidi kwenda kombo niliamua kuanza kupiga bei mali moja baada ya nyingine.
Nilianzia kuuza nyumba aliyokuwa kahongwa Neila, mwanamke aliyepigwa risasi na
kaka James.
Mara baada ya kuiuza
nyumba hiyo, niliyatangazia dau magari mawili ya kifahari yaliyokuwa yameachwa
na kaka James. Gari moja ni lile alilohongwa Neila; mwanamke aliyekuwa akijidai
ana mapenzi ya kweli kwa kaka James kumbe hamna chochote. Mwanamke ambaye
alisababisha kifo cha kaka yangu huyo.
Gari la pili ni lile
alilokuwa akitumia kaka James. Yote yalikuwa ni magari ya kifahari. Nilibakiza
gari moja ambalo nilikuwa nalitumia mimi. Hilo sikutaka kuliuza.
Ndani ya miezi sita
nilikuwa nimeshauza kila kitu; maduka, nyumba pamoja na kampuni ya
usafirishaji. Lengo langu lilikuwa ni kuhama kabisa mji huo.
Nilipomaliza michakato yote nilihama mji huo
na kuhamia mji mwingine ambako nilienda kununua nyumba na kuendelea na maisha
kama kawaida. Nilianza kufanya biashara zangu huko.
Nyumba hiyo ilikuwa
kubwa mno kukaa peke yangu kwani nilikuwa bado nahisi upweke kutokana na
kuondokewa na nguzo yangu muhimu katika dunia hii.
Ndipo nilipoamua
kukipangisha chumba kimoja na mpangaji aliyekuja kupanga alikuwa ni marehemu
Kishoka. Alikuwa ni kijana mstaarabu sana ambaye hakuwa na makuu.
Maisha yetu yalizidi
kuwa ya furaha kadri siku zilivyozidi kusonga. Tukawa tunaishi kama ndugu wa
damu ilhali tulikuwa tumekutana ukubwani tu kila mmoja akiwa na meno thelethini
na mbili.
Kiumri tulikuwa
hatupishani sana japokuwa alikuwa ananizidi miaka mitatu. Nilipomuita kaka naye
aliniita kaka. Pamoja na kunizidi umri lakini na mimi nilikuwa mwenye nyumba
wake.
Ilifikia wakati
nikamwambia asiwe ananilipa kodi ya nyumba kwani urafiki wetu ulikuwa umefikia
hatua nyingine. Akawa anaishi bila kulipa kodi ya pango siku zote.
Mpaka matatizo ya
kifo chake yanatokea tulikuwa tunaishi naye kama ndugu, kifo ambacho kilikuja
kikanigharimu hukumu ya kunyongwa nikisingiziwa kuwa mimi ndiye niliyemchinja.
Nilizidi
kuchanganyikiwa kwa kuona maisha yangu yakiandamwa na mikasa, mikosi na ndege
mbaya kila wakati. Kichwa kilizidi kuuma.
********************
ITAENDELEA.....
No comments:
Post a Comment