ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA....
Wakili
wa serikali bwana Charles Ngonyani alimtazama hakimu na kumwambia,
“Nimemaliza!” aliongea na kwenda
kuketi.
SASA ENDELEA.......
Ilifika
zamu ya wakili wa upande wa utetezi kumuhoji shahidi aliyekuwa kizimbani.
Wakili huyo bwana Jonas Mlyanyama alisimama na kusogea karibu na kizimba cha
shahidi wa upande wa mashitaka sajenti Bakari Mlongo.
“Umesema
mlipoingia chumbani mlimkuta mtuhumiwa anazunguka zunguka huku kisu kikiwa
kinaambaa ambaa sakafuni, si ndiyo?” Mlyanyama alimhoji shahidi huyo.
“Ndiyo!” alijibu na kumsikiliza wakili wangu
aendeleee kuongea
“Nikiiambia mahakama tukufu ya kwamba mteja
wangu alikuwa katika kustaajabu baada ya kulikuta tukio hilo limefanyika katika
chumba chake nitakuwa nakosea?”
“Ndiyo utakuwa unakosea kwa vile alama za
vidole zilionekana kwa mtuhumiwa baada ya kuchukua vipimo, yote hayo yatakuja
kuelezewa na mtaalamu wetu wa mambo ya picha na alama za vidole ambaye tulikuwa
tumeambatana naye siku hiyo.”
“Na ikiwa labda mtuhumiwa alikishika
kisu pamoja na mwili wa marehemu wakati tukio limeshafanyika ikiwa kwa
kutokujua au kutokana na kuchanganyikiwa na hali ya tukio lilivyokuwa?”
“Kwenye vipimo hatukuona alama zingine zaidi
ya alama za mtuhumiwa tu.”
“Huyo
aliyewapigia simu kituoni kuwapasha taarifa za tukio alikuja kituoni?”
“Hapana!”
“Mlichukua namba yake ya simu baada ya
kumaliza kuongea naye?”
“Hatukuweza kuchukua namba yake ya simu kwa
sababu alipiga kwenye simu ya mezani.”
“Mpaka jalada la upelelezi wa kesi hii linakamilika mtu huyo
aliwahi kufika kituoni japo mara moja nanyi mkapata kumfanyia mahojiano juu ya
tukio hilo?” Wakili Jonas Mlyanyama alimtwanga swali hilo tena shahidi wa
upande wa mashitaka.
“Hapana!”
“Sasa mimi naiambia
mahakama kuwa mteja wangu hakuua bali mwanamke huyo ndiye mbaya na huenda ndiye
aliyeua au anafahamu mwanzo mpaka mwisho juu ya mauaji ya Kishoka.”
“Siyo hivyo, mtuhumiwa ni yule pale kizimbani
kwa sababu hata alama zake zilionekana kwenye mwili wa marehemu na kwenye kisu
kinachosadikika kutumika kumchinja marehemu.”
“Sasa kwa nini mtoa
taarifa wa awali asijitokeze kituoni kutoa maelezo na kuwa tayari kuja kutoa
ushahidi mbele ya mahakama?”
“Kwa kweli hilo siwezi kujua ni kwa nini
hajaonekana kituoni.”
“Basi kubaliana na mimi ya kuwa yule ndiyo
mhalifu.”
Sajenti
Bakari Mlongo alionekana kuwa na kigugumizi hatimaye akaganda mithili ya cd
kongwe iliyochakaa. Wakili wangu bwana Jonas Mlyanyama alimwambia hakimu hana
la zaidi la kumuuliza shahidi huyo.
ITAENDELEA..........
No comments:
Post a Comment