ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA...
Baada
ya kuwaza kidogo alikumbuka kuwa bastola yake ilikuwa imebakiza risasi moja
ndani. Ndipo alipoamua kujimaliza na yeye kwa kujipiga risasi.
SASA ENDELEA.......
Wakati huo nilikuwa
namfuatilia kwani machale yangu yalikuwa yamenicheza. Wakati anaondoka nyumbani
alikuwa kashaniambia kuwa anaenda kwa mpenzi wake ila alikuwa akienda bila ya
taarifa huku akiyavunja masharti aliyokuwa amepewa na mpenzi wake huyo.
Niliamua kumfuatilia
ili nikashuhudie ‘timbwilitimbwili’ nililokuwa nikilitegemea kuibuka baada ya
kaka James kufika kwa mpenzi wake huyo. Hata kama yangetokea mapigano kisha
kaka yangu akazidiwa basi mimi ningekuwepo nyuma yake kuokoa jahazi.
Hata hivyo aliniacha
njiani kwani alikuwa akiendesha gari lake kwa kasi mno. Mimi nilikuwa naogopa
ajali hivyo nikawa naendesha mwendo wa kistaarabu.
Kwenda kwangu
polepole ndiyo kulinifanya nimkose kaka James katika dunia hii kwani
nilichelewa kiduchu mno. Wakati naufikia mlango wa chumba walichokuwamo kina
Neila, tayari kaka James alikuwa kashakitekenya kitufe cha kufyatulia risasi
huku akiwa amejilenga kwenye kichwa chake.
Nilimshuhudia kaka
James akianguka mzima mzima kisha akakata roho. Ndipo nilipopoteza fahamu na
kushindwa kuelewa kilichokuwa kikiendelea.
Fahamu zilinijia
masaa matano mara baada ya tukio hilo kutokea. Nilijikuta nipo wodini huku
nikiwa nimetundikiwa drip ya maji. Nilishangaa sana kujikuta nipo hospitali.
Katika kuvuta
kumbukumbu nilikumbuka jinsi mambo yalivyokuwa masaa matano yaliyokuwa
yamepita. Nilikumbuka kuwa kaka James hakuwepo tena duniani.
Nilizidi
kuchanganyikiwa, akili yangu ikazidi kuvurugika baada ya kukumbuka hilo tukio
lililokuwa na tanzia kubwa katika moyo wangu na akili yangu kwa ujumla.
Sikuona kabisa
mantiki ya kuendelea kubaki hospitali wakati nyumbani kulikuwa na msiba wa
marehemu kaka yangu. Sikujua ni vipi mipango ya mazishi ilikuwa inapangwa huko
kwani mimi ndiyo nilikuwa ndugu wa pekee wa marehemu. Kwa kifupi mhusika mkuu
wa msiba huo nilkuwa ni mimi.
Nilipojaribu kuangaza
angaza niliona karibu wagonjwa wote wamelala kwenye vitanda vyao kila mmoja.
Sikuona muuguzi wala dakitari yeyote aliyekuwemo kwenye wodi hiyo.
Bila kuchelewa wala
kuduwaa niliichomoa sindano ya drip na kutoka mbio kuelekea nyumbani kuungana
na majirani kuomboleza kifo cha kaka James.
Kwa vile James
alikuwa mtu mashuhuri sana katika mji huo, tayari taarifa za kifo chake
zilikuwa zimeshazagaa mtaani na katika mji wote kwa ujumla.
Nilipofika nyumbani
niliwakuta watu wengi wameshakusanyika. Hata hivyo mwili wa marehemu ulikuwa
upo hospitali umehifadhiwa kwa uchunguzi zaidi. Nilijumuika na watu waliokuwa
wameshafika, maombolezo yakaendelea.
Watu walizidi
kumiminika kuja kunipa faraja kwenye msiba huo. James alikuwa ni mtu wa watu,
alijua kukaa vizuri na majirani pamoja na watu wengine aliokuwa akifahamiana
nao. Hali ya watu kujaa ilinifariji kwa kiasi fulani ingawaje moyo wangu
ulikuwa umeghubikwa na majonzi yasiyokuwa kifani.
******************************
ITAENDELEA....
PESA/UTAJIRI WA NDAGU AU MAJINI KWA MUDA MFUPI
ReplyDeleteMPAKA MASAA 48(SIKU 2) PAPO HAPO ULIPO KUPITIA KALAMA KWA MASHARTI MAALUM KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......
HIZI NI DAWA NA MUDA WA UKAMILIFU WAKE NA KUKUKABIDHI
MAJINI ZIPO AINA 3
1. GHUUL(chma ulete)....Siku 5
2.SAIFRAHAN(Jini wa kufuga)...Siku 6 n.k
3.SAIFRAHA(jini wa bahati)....masaa 24
NDAGU ZIPO AINA 6
1.MTU.....week 1 na nusu
2.MIMBA....siku 5
3.UTASA....masaa 72(siku tatu)
4.ULEMAVU....siku tano
5.NDUGU WATATU...siku sita
6.WANYAMA.....masaa 48
KARIBU UPATE UFAFANUZI UCHAGUE UIPENDAYO KILA MOJA NA MASHARTI YAKE.
KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA
kwa maelezo kamili piga namba +255742162843
HACHA KUTANGATANGA PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI
NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI NA KUTUNZA SIRI......
NAITWA DR, MDIRO piga 0742162843. KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU ULINZI KWA MALI YAKO
(HUSITUME SMS PIGA SIMU KUHEPUKA MATAPELI)
MATIBABU MENGINEYO NI KAMA UTULIVU KATIKA NDOA, AU KUMVUTA UMPENDAE, KUONDOA MIKOSI, MABALAA, KUOSHA NYOTA, KUITAMBUA NYOTA YAKO NA ASILI YA KAZI YAKE, KAMA UNASUMBULIWA NA MAJINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI.
PIGA SIMU/Whatsup +255 742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA NA KUFATA MASHARTI. ANGALIZO USITUME SMS PIGA SIMU KUEPUKA MATAPELI