ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA......
Alinipa moyo na
kuniambia kuwa kwa vile nilikuwa sijafanya kosa hilo kama nilivyokuwa nimeshtakiwa,
Mungu angetusaidia na mwisho wa siku tungeibuka kidedea.
SASA ENDELEA.......
Baada
ya maongezi hayo yaliyochukua takribani saa moja wakili huyo aliondoka zake na
kuniacha nikirudishwa rumande kusubiri siku yingine ya kusomwa kesi yangu.
Niliendelea
na msoto wa rumande. Kila siku mlo mmoja kwa siku huku chakula chenyewe kikiwa
ni ugali wa dona na maharage yenye uozo. Maisha hayo nilikuwa sijawahi kuishi
hivyo ilikuwa ni vigumu sana kuyazoea.
Hata
hivyo sikuwa na jinsi, nililazimika kujikaza kisabuni huku nikisubiri kudura za
Wahidi ziniokoe katika hilo janga. Ilikuwa inauma sana hasa pale nilipofikiria
jinsi uhusiano wangu ulivyokuwa na mpangaji wangu Kishoka ambaye nilikuwa
natuhumiwa kumuua.
Tuliisha
kwa ushirikiano mkubwa kama ndugu wa damu ilhali tulikuwa tumekutana ukubwani
tu huku kila mmoja akiwa na meno thelathini na mbili; yaani akiwa mtu mzima.
Sikuhusika
na kifo chake, lakini nilikuwa nikishtumiwa ya kwamba nilimuua. Kwa mtindo huo
kwa nini sasa roho isiniume? Ilikuwa ni zaidi ya uchungu.
Siku
ya kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine tena iliwadia. Asubuhi asubuhi mimi
na mahabusu kadhaa tulisweka kwenye karandinga la askari magereza huku ulinzi
ukiwa umeimarishwa. Safari ya kuelekea mahakamani ilianza.
Mara
baada ya kufikishwa mahakamani tulishushwa huku tukilindwa kwa silaha za moto,
siraha nzito nzito za kivita. Mapaparazi nao walikuwepo kama kawaida yao,
wakaanza kutusonga ili wapate picha za kwenda kutuuzisha sura runingani na
magazetini.
Licha
ya kukaripiwa na askari magereza waliokuwa wametutanguliza, mapaparazi hao
walizidi kukomaa ‘kutufotoa’ na kamera zao. Tukaingia mpaka mahakamani tayari
kabisa kwa kuanza kusomewa mashtaka yetu kila mmoja kwa awamu.
Mimi
ndiyo nilianzia kupandishwa kwenye jukwaa la watuhumiwa kisha nikaapishwa kama
zilivyo taratibu za mahakama kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Baada
ya kuapishwa kizimbani kesi yangu ilitajwa. Hata hivyo jaji Aneth Mwalukwa
aliiahirisha tena kesi ili kusubiri jalada la kesi kutoka kwa mkurugenzi wa
mashtaka. Kesi yangu ilipelekwa mbele kwa muda wa majuma matatu.
Niliteremshwa
kizimbani na kurudishwa kwenye sello ya hapo mahakamani kusubiri mahabusu
wengine wamalize kusomewa mashtaka yao kisha turudishwe rumande.
Baada
ya mahabusu wengine kumaliza kusomewa mashtaka yao tulirudishwa rumande ya
magereza huku gari tulilokuwa tumepakizwa likikimbia kwa kasi.
ITAENDELEA......
No comments:
Post a Comment