ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA......
Nikiwa
rumande machozi yalizidi kunitiririka bila kukauka utadhani chemichemi za mto
Naili, chemichemi ambazo hutiririka bila kukauka misimu yote; iwe masika ama
kiangazi. Mifereji ya machozi ilikuwa inatiririka kutoka machoni ikipitia
mashavuni mpaka kwenye kidevu.
SASA ENDELEA.......
Mahojiano hayo
yalichukua takribani masaa mawili na nusu, hata hivyo hapakuwa na kipya zaidi
ya kurudia kuulizwa maswali niliyokuwa nimeulizwa hata kule hospitali. Pia
katika mahohjiano hayo yaliambatana na vitisho lukuki vya kunitaka nikiri kuwa
nilimuua Kishoka. Hata hivyo niliendelea kushikilia msimamo ya kuwa sijaua.
“Wewe ni muuaji ila
unajifanya ni mbishi, mbona ripoti ya postimotamu imeonyesha kuwa wewe ndiyo
umeua?”
“Hapana afande, mimi sijamuua Kishoka. Maelezo
niliyoyatoa ndiyo yana ukweli wote.”
“Mbona kwenye kisu kilichotumika kumuulia
marehemu tumeona alama za vidole vyako, vilevile kwenye mwili wa marehemu alama
za vidole vyako zipo?”
Hilo
nalo lilikuwa ni neno. Nilishtuka sana kusikia hivyo. Ukweli ni kwamba wakati
naingia chumbani kwangu sikujaribu hata kukigusa kisu kilichotumika kumchinja
Kishoka. Isitoshe hata mwili wake sikuugusa; sasa jambo la alama zangu za
vidole kuonekana kwenye kisu hicho na kwenye mwili wa marehemu lilizidi
kunichanganya. Wakati mwingine nilihisi huenda ni mitego tu ya makachero hao
ili kumfanya mtu aropoke kama kweli katenda kitendo hicho.
“Hilo
ni jambo geni kwangu, kile kisu sikuwahi hata kukigusa zaidi ya kukitumbulia
macho. Hata mwili wa Kishoka sikuwahi kuugusa zaidi ya kuukodolea macho, sasa
alama za vidole vyangu zilifikafikaje kwenye kisu na maiti ya Kishoka?”
“Unatuuliza tena sisi! Naona wewe huna jipya
ila ni ubishi tu unaokusumbua. Kesho faili lako tunalipeleka mahakamani kwani
uchunguzi wetu sisi umeshakamilika.” Alimalizia kuongea askari huyo aliyekuwa
amevaa nguo za kiraia kisha akaamuru nirudishwe rumande.
Baada ya mahojiano
hayo nilirudishwa tena rumande. Kilichokuwa kinasubiriwa pale ni kufika asubuhi
nyingine kisha nipelekwe mahakamani kujibu shauri lililokuwa likinikabili.
Nilisweka tena ndani na kuanza kuburudika na
adha ya humo. Joto la kufa mtu nilikuwa linanisumbua kwa wakati huo. Hamkuwa na
mkeka wala busati hivyo nililazimika kujilaza kwenye sakafu.
Ilipofika jioni mbu
walicharuka tena. Ikawa tafrani mtindo mmoja, usiombe mbu wa rumande ndugu
msomaji, wanauma mpaka kwenye nyayo. Nahivi sikuwa na shuka wala blanketi,
heheee, nakwambia nilikoma kuringa.
Asubuhi nyingine
ilifika japokuwa kwa shida sana. Mbavu zote zilikuwa zikiniuma kutokana na
kulala kwenye sakafu usiku kucha. Mikononi na niguuni vilikuwa vimejitokeza
vipele vingi kutokana na kutafunwa na mbu usiku mzima.
Mara mlango wa selo
ulifunguliwa kisha nikawaona askari watatu wakinitaka nitoke. Nami bila ubishi
nilitoka. Nilipotoka tu hawakunichelewesha, wakanifunga pingu kisha
wakanipeleka sehemu ambako kulikuwa na karandinga.
Waliniamru
nipande nami nikajitoma bila ya ubishi. Safari ya kuelekea mahakamani ilianza.
Gari lilitoka mbio utadhani lipo katika mashindano, tulitumia takribani dakika
kumi kufika mahakamani.
HAYA SASA BRIGHTON KASHAFIKISHWA
MAHAKAMANI KWA MARA YA KWANZA. JE, KESI YAKE ITAENDAJE?
No comments:
Post a Comment