ILIPOISHIA........
“Utanisamehe
kaka yangu kwa sababu nina haraka kwelikweli, ila usijali, nitakuja kwako kesho
asubuhi!” Alinijibu bila ya kugeuka kuniangalia.
SASA ENDELEA.......
Niligutushwa na kauli yake hiyo, kauli ya kwamba atakuja kwangu kesho
asubuhi. Akili yangu ilianza kuwaza mara mbilimbili bila kupata jibu.
‘Nimeiona sura yake kwa macho yangu mawili ya
damu na nyama, tena mchana kweupe lakini sijamfahamu, sasa iweje yeye awe
anapafahamu mpaka nyumbani kwangu?’ Nilizidi kuwaza.
Nilimuuliza
kama anapajua ninapoishi naye akasema anapajua. Nikamuuliza kama ananifahamu
mimi, akanijibu kuwa ananifahamu, tena kwa kukata mzizi wa ubishi alinitajia
hadi jina langu,
“wewe si unaitwa Brighton mdogo wake na
marehemu James!” nilizidi kuchoka.
Chaajabu
maongezi yetu yalikuwa yanafanyika huku tukiwa tunatembea, yeye yupo mbele na
mimi nipo nyuma, nikajaribu kumbembeleza ageuke ili nimuangalie kwa makini
huenda na mimi ningemtambua lakini hakukubali.
‘Huyu
mrembo mbona simuelewi? Anadai ananifahamu, kwa nini sasa asisimame japo kidogo
tusalimiane? Kama ananifahamu kweli na pia anapafahamu ninapoishi, kwa nini
asisimame japo dakika sifuri tukasabahiana kisha akaendelea na safari yake?’ Niliwaza
na kuwazua huku nikiendelea kuchapa lapa nikiwa nyuma ya mlimbwende huyo.
Nilitembea
kwa takribani dakika kumi nikimfukuzia msichana huyo lakini alikuwa hajakubali
kunisubiri au kugeuka kuniangalia. Hakutaka kabisa kunielewa kwani kujikomba
kwangu kote ilikuwa ni sawa na kumuimbia kiziwi ama kummulikia kipofu.
Niliamua
kuachana naye huku nikijipa matumaini kuwa kesho siyo mbali,
‘tena si kasema mwenyewe kuwa atakuja kunako
anga zangu? Hahaaaa!’ Nilijikuta nikiangua kicheko cha dharau huku nikigeuka
nyuma kuanza kurudi ufukweni.
Nilitafuta
mahali palipokuwa pametulia ili nijipumzishe, nieendelee kufurahia upepo murua
unaovuma bila bughudha kandokando ya bahari.
Mawazo
ya ndoto ambayo nilikuwa nimeiota masaa machache kabla ya kwenda ufukweni yalianza
kupotea. Nikaanza kuamini usemi wa baadhi ya watu wanaodai kwamba ufukweni ni
sehemu ya kupotezea mawazo na kutuliza akili. Kwa wakati huo usemi huo nilikuwa
siutilii shaka hata kidogo.
Kichwa
changu sasa nilianza kukiona ki chepesi, uzito kiliokuwa nao mara baada ya
kugutuka kutoka ndotoni nikawa siuhisi tena. Niliamua kuanza kurudi nyumbani
kwani machweo nayo yalikuwa yamewadia.
*******************************
JE, HUYO NSICHANA NI NANI NA
KAMJUAJE BRIGHTON? USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA.........
No comments:
Post a Comment